Kisiwa cha Antelope

40°57′N 112°13′W / 40.95°N 112.21°W / 40.95; -112.21

Ramani ya Mbuga ya kisiwa cha Antelope
Kundi la baisani katika kisiwa cha Antelope
Shamba la Fielding Garr katika kisiwa cha Antelope .
Pwani ya kisiwa cha Antelope kutoka kwenye njia iliyo juu ya maji.
Maeneo ya mawimbi kutoka Ziwa Bonneville (Pleistocene) katika kisiwa cha Antelope , ziwa kuu la chumvi, Utah.

Kisiwa cha Antelope (kwa Kiingereza: Antelope Island) ni kisiwa cha Marekani. Kipo ndani ya Ziwa Kuu la Chumvi (Great Salt Lake) katika Jimbo la Utah. Hili ni ziwa la chumvi kubwa zaidi katika Marekani [1] na ziwa kubwa la maji ya chumvi katika Bara la Amerika [2]. Eneo la kisiwa ni square mile 42 (km2 109).

Kiutawala kisiwa hiki kiko ndani ya Kata ya Davis, katika sehemu ya kusini ya ziwa na kuwa eneo linalostawi wakati ziwa liko katika kiwango cha chini.

Kisiwa cha Antelope huwa na paa, nungunungu, melesi, koyote, linxi mkia-mfupi, kondoo pembe-kubwa, baisani wa Amerika 600 na mamilioni ya ndege wa maji. Baisani alikaribishwa katika kisiwa hiki mwaka wa 1893, na kuwa na kudhibitishwa kuwa eneo la uzalishaji wa baisani kwa makusudi ya kuhifadhi.

  1. Czerny, Peter G. (1976). Ziwa kuu la chumvi. Provo, Utah: Kundi la uchapishaji la chuo kikuu cha Brigham. ISBN 0-8425-1073-7
  2. www.utah.com / stateparks / great_salt_lake.htm

From Wikipedia, the free encyclopedia · View on Wikipedia

Developed by Tubidy